Mambo niliyojifunza katika kitabu cha THE COMPOUND EFFECT cha mwandishi DARREN HARDY.
Habari ndugu msomaji wa makala hii!
karibu tuendelee kujifunza ili kuweza kwenda sawa na maish.a ya sasa yasiokwisha changamoto.
As long as you live,keep learning how to live-Lucius Annaeus Senneca.Mwanafalsafa huyu anatuambia"kwakuwa tunaishi,basi hatuna budi kujifunza namna ya kuishi"
Maisha
uliyonayo sasa ni matokeo ya mambo mbalimbali madogo madogo uliyoyafanya huko
nyuma,maisha yoyote yale uliyo nayo kwa
sasa,ikiwa ni mazuri au mbaya,bas jua ni
matokeo.
Twende
moja kwa moja rafiki tukaangazie yale
niliyojifunza kwenye kitabu tajwa hapo juu;
- Hatua ndogo na makini unazochukua katika maisha yako zinakupelekea katika mafanikio makubwa.Ni ukweli usiopingika kuwa mafanikio ni matokeo,sasa ili upate matokeo mazuri kuna mambo mengi unayotakiwa kuyafanya ili uweze kupata matokeo hayo,na mambo hayo wala si makubwa sana ,bali yanafanywa kwa muda mrefu mno mpaka yanakuwa utamaduni au tabia na mwisho huleta matokeo makubwa.
- Kufanya kazi kwa bidii bila kukata tamaa kunalipa sana.Binadamu tunapenda matokeo ya papo kwa hapo,yani nipe nikupe,ufanye kazi halafu baada ya kazi ulipwe mara moja.sasa mafakio hayako hivyo,bali yanakutaka ufanye kazi kwa bidii sana tena muda mrefu bila kukata tama ndipo utakapoona matunda mazuri yakile unachofanya.
- Kila chaguo unalofanya katika maisha yako basi lina athiri moja kwa moja matokeo au mafanikio yako makubwa.Hivyo chagua kilicho bora kwako.
- Mfulilizo wa hatua ndogo ndogo mbaya unazochukua zinakupelekea katika katika maangamizi na majuto makubwa.kama ilivyo kwamba mafanikio ni matokeo,basin a majuto pia ni matokeo.mkusanyiko wa makosa yako mengi katika Nyanja tofauti za maisha yako ndio huleta majuto.
- Jitoe kwa asilimia mia moja bila kutaraji kupata kutoka kwa wengine,wapende wengine kwa asilimia mia moja bila kujali wao wanakupenda kwa kiwango gani au labda hawakupendi kabisa.
- Chukua jukumu la maisha yako kwa asilimia mia moja,usitegemee mcahngo kutoka kwa mwingine au yeyote isipokuwa kutoka kwako wewe mwenyewe.Usiilaumu serikali kwa kutokuajiri,hakika serikali haiwajibiki katika kufikia ndoto zako,na hata kama inawajibika,basi sikwakukupa ajira bali nikwa namna nyingine ambayo huwenda imeshatekeleza.Pia baba yako ama ndugu yako yeyote hawajibiki katika kufikia malengo uliyojiwekea isipokuwa wewe mwenyewe.
- Tofauti kati yakuwa tajiri au kuwa na furaha na kutokuwa na furaha ni hatua au maamuzi uliyoyafanya katika kipindi Fulani cha maisha yako.Na si kitu kingine
- Kila mtu ana nafasi ya kuwa na bahati,kama unaishi katika jamii iliyo huru tayari una bahati.bahati ni pale fursa inapokutana na maandalizi.
KANUNI
ya kutengeneza bahati
Maandalizi(Ukuaji
binafsi)+Mtazamo+Nafasi/fursa+hatua(fanya jambo)=BAHATI.
9 Bahati zinatuzunguka kila tulipo,ila huwez kuona kile ambacho hujakitafuta,na huwez kutafuta
kile ambacho huamini uwepo wake.Pamoja na kwamba bahati zinatuzunguka,ni lazima uitafute ndipo utaiona.na ili utafute kitu lazima uamini kwamba kipo.
9 Bahati zinatuzunguka kila tulipo,ila huwez kuona kile ambacho hujakitafuta,na huwez kutafuta
kile ambacho huamini uwepo wake.Pamoja na kwamba bahati zinatuzunguka,ni lazima uitafute ndipo utaiona.na ili utafute kitu lazima uamini kwamba kipo.
10 “The
day you graduate from childhood to adult hood is the day you take full
responsibility of your life”Jim Rohn“Siku ambayo unahitimu kutoka hali ya utoto
kuingia hali ya utu uzima ndio siku ambayo unabeba mustakabali mzima wa maisha yako.
11 Chukua
hatua sahihi kila siku,kila wiki na kwa miaka,na utashuhudia namna utavyokuwa
kiuchumi.kama tulivyoona kuwa matokeo makubwa huletwa na hatua ndogo ndogo
ambazo umekuwa unazichukua na kuzifanya kama tabia.
12 Wekeza asilimia kumi
ya kipato chako au kila kinachopita katika mikono yako.hapa sio lazima
uwe
umeajiriwa nakupokea kila mwisho wa mwezi,hapana.kinachotakiwa nikuhakikisha
kila fedha unayoipata labda nifaida katika biashra zako,au malipo yako ya kila
siku katika kileunachofanya
13 Jambo
la msingi nikuanza sasa.usisubiri mpaka uwe tayari ndio uanze,kwani hakuna siku
utakuwa tayari kuanza bali kila siku utajiona bado hujawa tayari au kuna
mapungufu yanakuzuia.
14 “We
are what we repeatedly do”Aristote.tulivyo ni matokeo ya yale tunayofanya mara
kwa
mara.Sasa ili uwe bora hakikisha unachukua hatua sahihi mara kwa mara.
15 Watu
wanaendeshwa na tabia zao bila hata kujua zinawapeleka wapi.tabia
tulizojijengea ndio
zimekuwa muongozo wetu bila hata ya kujua ni wapi
zinakotupeleleka.yapeleke maisha yako
katika muelekeo unaotaka.
16 kuwa
na viatu vizuri kwa ajili ya mbio za marathon,haitoshi kuwa sababu ya kwamba
tuko tayari kwa kuanza mashindano.
17 Haitoshi
tu kuchagua kuwa na mafanikio,
18 Unajua
ni kipi kinachokuzui kurudi nyuma na kutumbukia katika tabia mbaya ulizokuwa
nazo?kuna tabia ambazo uligundua nikikwazo kwako katika kufikia hatua
ulizojiwekea malengo nakuamua kuzipiga vita.basi unatakiwa ujue kipi kinakuzuia
usirudie tabia izo.
19 Usikazanie
mafanikio peke yake bali kutosheka kunakufanya uwe na furaha zaid katika maisha
yako.kutosheka na kile ulichonacho kutakufanya uwe na furaha na uyafurahie
maisha.kutosheka haina maana usiendelee kutafuta bali kushukuru na kuendelea
kuweka juhudi.
20 Mafanikio
makubwa hayakuhakikishii kuwa na furaha zaid.furaha inatakiwa itoke ndani yetu
na isitegemee vitu vya nje.usitarajie ufanikiwe kwanza ndo uwe na furaha,bali
tengeneza furaha kwanza ndio mafanikio yafuate,
21 Maadui
zetu wanatupa sababu ya kusimama na kusonga mbele kwa hamasa kubwa.usiogope
watu wanaokupinga au kukuchukia katika lile unalofanya,kwani wanakufanya uzidi
kuwa nasababu za kufanikiwa
22 Unapoilekeza
akili yako katika kile unachokitafuta basi utakiona.hakika dunia ina kila kitu
unachohitji,bali ili ukipate lazima uweke juhudi kubwa katika kukipata.
Kanuni
tano za kufuata ili uweze kuondoa tabia
mbaya ulizonazo.
ü Vitambue
vichocheo vyako.
Tambua vichocheo
vinavyokusukuma katika tabia hiyo mbaya,mfano,mara nyingi unakunywa pombe
unapokuwa na watu wa aina Fulani?
ü Safisha
nyumba
Maana yangu hapa ni
hii,kama unataka kuacha pombe basi ondoa chupa zote za pombe na vitu vyote
unavyotumia wakati wakunywa pombe ndani ya nyumba yako na eneo lako la kazi.kama
unataka kuachana na tabia mbaya ya matumizi ya hovyo ya pesa,basi tumia jioni
yako katika mambo mengine ya msingi na futa ofa zote unazopokea za kukuomba
kujumuika katika maeneo ya starehe.
ü Badilisha.
Angalia tabia zako zote
mbaya,je unaweza kuzibadilisha kwa kitu kingine chenye faida?mfano pale
unajiskia kuvuta sigara tafuta kitu kizuri cha kutafuna kwa muda huo ambacho
hakina madhara kwa afya yako.
ü Rahisisha
Baadhi ya tabia zako
mbaya umezijenga kwa muda mrefu kiasi kwamba huwezi kuziondoa mara moja,basi
usikazane kuziondoa mara moja bali jipe muda.
ü Ruka.
Badili tabia zako zote mbaya kwa
wakati mmoja.
23. Hutaweza
kamwe kubadili maisha yako mpaka ubadili yale unayoyafanya kila siku.kama
tulivyokwisha ona kuwa maisha ni matokeo ya hatua unazochukua kila siku,kwaiyo
ili ubadli maisha yako lazima ubadili yale unayofanya kila siku.kwani siri ya
mafanikio yako iko ndani ya maisha yako ya kila siku.
Kanuni sita zakukusaidia kujijengea
tabia nzuri.
a. Jiweke
kimafanikio.
Ondoa au jiweke mbali
kabisa na vile vitu ambavyo vinaweza kuwa kikwazo katika safari yako ya
mafanikio.na jijengee zile tabia ambazo waliofanikiwa katika jambo ilo wanazo.
b. Fikiria
sana katika kuongeza na si kupunguza
Mara nyingi wekeza
zaidi fikra zako katika kile unachotaka kuongeza na sikile unachotaka kuondoa
c. Iambie jamii kwamba umebadilika,
unapojua kuwa kuna watu
wanakufuatilia mwenendo wako,ni vigumu kurudi kwenye tabia mbaya ambayo ulikuwa
nayo na kuwaambia familia,rafiki kuwa umeshaiacha.mfano,kama ulikuwa unavuta
sigara,kisha ukawaambia rafiki na ndugu kuwa umeacha kuvuta sigara,basi itakuwa
rahisi wewe kuacha kuvuta sigar kwakuwa unajua nikivuta kuna watu wataniona.
d. Kuwa na rafiki mwenye ndoto kama
yakwako,
kuwa na rafiki ambaye
atakuwa anakuhamasisha nakukumbusha katika utaratibu mliojiwekea.mfano rafiki
ambaye mmepanga mkutane kila siku muda Fulani kwa ajili ya mazoezi.
e. Fanya mashindano,
kawaida unapojua kuwa
uko kwenye mashindano,basi unaweka juhudi ili uweze kuibuka mshindi.ni aina
gani ya mashindano unaweza ukafanya na marafiki zako?
f. Jipongeze,
sasa ni muda wa kujipongeza kwa
kufurahia matunda ya ushindi wako.unaweza fanya hivyo kwa namna mbalimbali kama
kusoma kitabu kwa ajili ya kujifurahisha au kwenda kutembea
24 Kufanya mambo kwa Kawaida ni rahisi,kufanya
mambo katika ubora wa hali ya juu ndicho kitakachokutenganisha na kundi kubwa
la watu.binadam hatupendi sana kuwa peke yetu au kuwa tofauti na wengine,hii
inatupelekea kufanya vitu kama wengine wanavyofanya na mwisho kupata matokeo
yakawaida kabisa,ni pale tu utakapofanya katika ubora ndipo utakapo
jitofautisha na kundi kubwa la watu.”The ultimate measure of man is not where
he stand in moment of comfort and convenience,but where he stands at time of
challenges”Martin luther
25 Jipe
muda katika kubadili tabia zako mbaya ambazo umezijenga na kuziishi kwa muda
mrefu.tabia hizi unatakiwa kuzibadili taratibu taratibu kwa kuwa zimeshakita
mizizi katika maisha yako.
26 Kufikia
malengo mapya uliyojiwekea na kutengeneza tabia mpya ni muhimu kuwa na mfumo
utakaokusaidia kuyatimiza hayo.binadam kawaida hatupendi sana kubadilika,sasa
ili usirudi kwenye mzoea yako ni lazima kuwe na namna yakukusaidia katika hilo.
27 Fikiria
mambo yote ambayo unapaswa kushukuru kwayo.kuna wakati huwenda ukahisi maisha
yako hayana maana,nikwasababu hujakaa chini na kutafakari zile neema nyingi
ambazo Mwenyezi Mungu amekupa.na hii nikwasabab umeelekeza sana fikra zako
katika uliyokosa na si yale uliyonayo.
28 Namna
ya kupata kutoka kwa wengine ni wewe kutoa kwanza.ili upate upendo kutoka kwa
wengine waonyeshe kwanza waonyeshe kwanza wewe upendo.
29 Akili
huwa inaendelea kuchanganua taarifa za mwisho ilizopokea kabla ya kulala.hivyo
ni muhimu kuilisha akili yako taarifa za msingi na chanya kabla ya kulala.
30 Unashinda
pale unapochukua hatua sahihi kila siku,ila unajiweka katika hatua ya kushindwa
pale unapohitaji matokeo ya haraka sana.
31 Kila
mtu anaathiriwa na vitu vitatu.
ü Unachopokea,kipi
unaweka katika kichwa chako.
ü Unaofungamana
nao,wale ambao muda wako mwingi unautumia ukiwa nao.
ü Mazingira,mazingira
yanayokuzuka.
32 Ubongo
wako haujatengenezwa kwa ajilinya kukupa furaha.upo kwa ajili ya kuratibu mambo
mbalimbali yakukuwezesha kuishi,kwani ubongo ukifa na wewe unakufa.
33 Kichwa
chako ni kama glass iliyo tupu,inapokea chochote utakachoweka.kwa maana hiyo ni
muhimu kuweka yale yenye kukunufaisha na yenye kukujenga kuwa mtu chanya katika
maisha yako.
34. Vyombo
vya habari mara nyingi hukupa taarifa za kusikitisha na kusisimua ili kukutoa
kwenye hali yako ya utulivu na mazingatio.
35 Huwezi
amabatana na watu ambao ni hasi mara lkwa mara halafu ukategemea kuwa chanya.
36 Kile
unachokivumilia katika maisha ndicho unachokipata,kama unavumilia kulipwa
mshahara mdogo na kufanya kazi nyingi,hilo ndilo litakaloendelea kwako.
37 Hamasa
bila yakuchukua hatua ni sawa na kujidanganya mwenyewe.
38 Wazo
lisilofanyiwa kazi limekwishapotea.
Hayo
ndio niliyojifunza rafiki katika kitabu hiki.hakika yapo mengi mno ya
kujifunza,nakushauri utafute kitabu hiki ili uweze kujifunza zaidi.
Nikutakie
safari njema ya mafanikio
Rafiki
yako Elishad Bashiru.
Comments