ISHUKURU SANA JANA YAKO
"Use the lessons you have learned from your past to rise to a whole new level of awareness and enlightenments"Robin Sharma. Habari rafiki!kwanza kabisa hatuna budi kumshukuru Yule aliyetuwezesha kuiona siku hii mpya ambaye ni Mwenyez Mungu Muumba mbingu na ardhi.Hatuna budi pia kuitumia siku hii kuongeza thaman katika Maisha yetu,kwani ni wengi walitamani wawepo ila hawapo. Karibu sana rafiki.hakika Jana yetu imetawaliwa na mambo Mengi yakiwemo mabonde na milima, makosa na Maudhi pamoja na usaliti mbali mbali lakini yalishapita na Leo tuko katika wakati Wa sasa.Jana yetu ina nafasi kubwa ya kujenga au kuharibu maisha yetu ya sasa.Pale utakapoanza kujilaumu Kwa makosa ambayo uliyafanya na kukupa matokeo mabaya na kukupa wakati mgumu,pale utakapoanza kuwalaumu watu Kwa Yale waliokufanyia mabaya na kujipa sababu kuwa wao wamekuharibia maisha,basi umeamua kupoteze nguvu na muda wako wa sasa kwenye wakati uliopita.Na huo ni uamuzi mbaya Sana katika Maisha yako.Uamuzi sahihi ni ...