MAISHA


Kuna wakati katika Maisha unapitia mambo  magumu sana, na kila ukijaribu kuondokana na hali hiyo bado hupati majibu sahihi.
Nikuambie rafiki, huo ndio wakati unatakiwa kuishi hali hiyo Kwa MUDA!huwa tunasahau kuwa MUDA nao ni tiba ya matatizo yetu.Yape matatizo yako MUDA.
kama vile unavyoweza kuipenda nyumba ilihali imefungwa na hujui kilichopo ndani, basi yapende matatizo yako uliyoshindwa kuyatatua.
Kuna watu wanapenda nyimbo japo zimeimbwa Kwa Lugha wasioifahamu,kwanini usiipende Hali uliyonayo Kwa MUDa?

Kumbuka kila Hali unayopitia Mungu anamakusudi juu yako,huwenda hata matatizo yako yakiondoka sasa hutaweza kuyafurahia Maisha Au hutaweza kuishi katika Hali hiyo tulivu yakukosa changamoto.

Nikutakie siku mpya yakuyaendea mafanikio rafiki yangu.

Elishad bashir
Irshady12@gmail.com.

Karibu tujifunze zaidi kwenye
amkanauishi.blogspot.com.

Comments

Popular posts from this blog

SARATANI YA MATITI

Mambo niliyojifunza katika kitabu cha THE COMPOUND EFFECT cha mwandishi DARREN HARDY.

Uchambuzi Wa kitabu;MAMBO 12 Niliyojifunza katika kitabu cha THE BOOK OF HAPPINESS.