MAMBO NILIYOJIFUNZA KATIKA KITABU CHA BLESSED IN DARK PLACES.BY Joel Osteen.
katika maisha watu huwa kuna wakati wanapitia vipindi vigumu.Katika vipindi vigumu ndio wakati ambao mtu huhisi kwamba dunia
haimtaki tena na Mungu pia amemsahau.Pia wakati huu ndio wakati ambao mtu
huhisi kwamba yeye ndo basi tena,na hawezi tena kurudi katika maisha yake ya
mwanzo.
Ila ukweli hauko hivyo,kwani ni katika vipindi vigumu ndipo
hutokea washindi.Watu wengi waliofanikiwa katika jambo fulani,ukifuatilia
utakuta kuwa walipitishwa kwanza kwenye wakati mgumu ndio yakapatikana matokeo
ambayo wengi tunayaona.Mara nyingi tunaangalia matokeo ndio maana tunahisi
fulani ana bahati na wewe huna,lakini nyuma ya bahati kuna mchakato amepitia.
Mwandishi Joel Osteen ameelezea mambo makubwa sana katika
kitabu chake cha Blessed in the Dark Places.Haya hapa ni baadhi tu ya mambo
niliyojifunza kwenye kitabu hicho kutoka ukurasa wa 1-45.
1.Usilalamike sana
unapopitia wakati mgumu kwenye maisha yako,huo wakati mgumu ndio Mungu huutumia
kupitisha neema zake kwako.
Kwenye wakati huu kikubwa kinachohitajika ni subira na
imani juu ya Mwenyezi Mungu,amini kwamba kipindi hicho ni chenye kupita,na hata kama kisipopita bado unatakiwa uaminifu wako kwake usitetereke.
2. Wakati mgumu ni
sehemu tu ya mpango wa kutaka kuibua kile kilichopo ndani yako.
Kila mtu ana kitu ndani yake ambacho Mungu amekiweka,lakini
mara nyingi kitu hicho hakiwezi kujionyesha mpaka mtu huyo apitie kipindi
kigumu kitakachomuhitaji ajitathimini sana na kutumia akili nyingi
navipawa vyake.kama ilivyo mbegu haiwezi kuota mpaka ifukiwe ardhini kwenye
giza,joto,maji na kila aina ya karaha.
3. Mungu hualipisha
watu kwa yale mabaya waliowafanyia wengine.
Kuna watu wanaweza kukufanyia mabaya na kukusababishia
machungu kwenye maisha,lakini Mungu humlipa mtu kwa yale mabaya aliofanyia
wengine.waswahili husema “Malipo ni hapa hapa duniani”
4. Changamoto
unayopitia inaweza kuonekana kubwa na usioweza kupambana nayo.Ila kumbuka kwa Mwenyezi Mungu hakuna linaloshindikana.
Haijalishi changamoto unayopitia ina ukubwa gani,ukimuamini
Mungu kwa uwezo wake hakuna linaloshindikana.
5.Huwenda kwasasa uko kwenye wakati mgumu shida na taabu
zinakuandama,ila kumbuka hicho ni kipindi cha mpito tu,kuna kitu Mungu anafanya
juu yako na utakuja kukishuhudia.
6.Usikubali changamoto za maisha zikutoe kwenye lengo na kukata tamaa katika zile ndoto zako kubwa
ulizo nazo,hakika changamoto zipo tu,kwaiyo zenyewe sio tatizo sana,tatizo ni
wewe namna unavyozipokea.
7.tabia njema za mafanikio hujengeka kwa mtu pale anapopitia kipindi kigumu na mambo yake hayaeleweki,ila akaendelea kufanya yale yaliyo sahihi na yamuhimu.
8.Mungu huwa hakupitishi kwenye njia nyepesi na
yawazi,anakupitisha kwenye njia ngumu inayoambatana na kupoteza vile vyenye
thamani kwako,kukataliwa,kuvunjwa moyo,kuachwa na kila aina ya mateso.Na yote
hayo ni sehemu ya mipango yake juu yako.
9.wakati mwingine vikwazo na kuvunjwa moyo ni sehemu ya
majaribu,Mwenyezi Mungu anataka kujua je utaendelea kumuamini hata kipindi
ambcho mambo yako yanaenda hovyo?.
Hayo ndio baadhi ya mambo niliyojifunza mwanzoni kabisa mwa
kitabu hiki kizuri kabisa kinachokujengea ujasiri wa kuishi na kufurahia maisha
hata kama uko kwenye akati mgumu.Kinakufanya uitue mizigo uliyoibeba na kuikabidhi
kwa Mwenyezi Mungu ambaye hashindwi na lolote chini ya jua.
Elishad bashiru
Comments